65. KATIKA SAFARI YETU

KATIKA SAFARI YETU

1.  Katika safari yetu
Kwenda Mbinguni
Tusiishe siku zetu
Usingizini.

Chorus:
Ng’oani! Tujifungeni,
Twende zetu juu!
Kristo ndiye kiongozi;
Tusihofu tu.
 
2.  Atwekwe badala yetu,
Mwenyewe Bwana;
Yesu kiongozi wetu
Atapokea.
 
3.  Kisimani, maji tele,
Maji mazima!
Maji hayo,
Ya milele
Yana neema.
 
4.  Njiani miiba mingi,
Yatuumiza;
Hofu na hatari nyingi,
Sana zakaza.
 
5.  Kweli, njia ya Mbinguni
Ni ya mashaka;
Tuwe na Yesu njiani,
Mara hufika.

Comments

Popular posts from this blog

67. BWANA ULIYEWAITA

68. MUNGU MSAADA WETU

81. CHINI YA MSALABA