73. YESU ZAMANI BETHILEHEMU

YESU ZAMANI BETHILEHEMU

1.  Yesu zamani Bethilehemu,
Aliyezaliwa kwa aibu,
Ndiye mwakozi wa ulimwengu,
Akaja kwa mimi.
 
Chorus:
Akaja kwa mimi; akaja kwa mimi;
Ndiye mwaokozi wa ulimwengu,
Akaja kwa mimi.
 
2.  Yesu akafa msalabani,
Kuniponya akalipa deni,
Ni la ajabu ya jinsi gani
Kunifia mimi!

Chorus: 
Kunifia mimi! Kunifia mimi!
Ni la ajabu ya jinsi gani
Kunifia mimi.
 
3.  Ni Yeye huyo tangu asili;
Na nilipotanga-tanga mbali
Alikuja kwa upole, kweli
Kuniita mimi.
 
Chorus:
Kuniita mimi; Kuniita mimi;
Alikuja kwa upole, kweli
Kuniita mimi.



4.  Yesu kristo atarudi tena,

Hilo lanifurahisha sana.

Yeye Bwana akionekana

Kunijia mimi.

 

Chorus:

Kunijia mimi, kunijia mimi,

Yeye Bwana akionekana

Kunijia mimi.

Comments

Popular posts from this blog

67. BWANA ULIYEWAITA

68. MUNGU MSAADA WETU

81. CHINI YA MSALABA