77. MSALABANI PA MWOKOZI

MSALABANI PA MWOKOZI

1.  Msalabani pa mwokozi,
Hapo niliomba upozi,
Akaniokoa mpenzi,
Mwana wa Mungu.

Chorus:
Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,
Akaniokoa Mpenzi, Mwana wa Mungu.
 
2.  Chini ya mti msumbufu,
Niliomba utakatifu,
Alinikomboa kwa damu,
Mwana wa Mungu.

Chorus: 
Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,
Alinikomboa kwa damu, Mwana wa Mungu.
 
3.  Aliniokoa dhambini,
Ikawa kunikaa ndani,
Aliponifia mtini,
Mwana wa Mungu.
 
Chorus:
Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,
Aliponifia Mtini, Mwana wa Mungu.
 
4.  Damu ya Yesu ya thamani,
Huniokoa makosani,
Huniendesha wokovuni,
Mwana wa Mungu.

Chorus: 
Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,
Huniendesha wokovuni, Mwana wa Mungu.
 
5.  Hicho kijito cha gharama,
Leo jivike kwa kuzama,
Kwake uuone uzima,
Mwana wa Mungu.

Chorus: 
Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,
Kwake uuone uzima, Mwana wa Mungu.

Comments

Popular posts from this blog

67. BWANA ULIYEWAITA

68. MUNGU MSAADA WETU

81. CHINI YA MSALABA